Miss Tanzania 2014 aliyevuliwa taji, Sitti Abbas Mtemvu akipanda jukwaani kupata maombi ya Nabii Yaspi Bendera.
Stori: Chande Abdallah, Deogratius Mongela na Musa Mateja.
TENA! Saa chache tu baada ya Miss Tanzania 2014 aliyezua tafrani la kuchakachua umri kwa kujipunguzia miaka 2 ya kuzaliwa, Sitti Abbas Mtemvu kujisalimisha kwa kujivua taji mwenyewe, mapya yameibuka na Ijumaa Wikienda lina mzigo mkononi!
TENA! Saa chache tu baada ya Miss Tanzania 2014 aliyezua tafrani la kuchakachua umri kwa kujipunguzia miaka 2 ya kuzaliwa, Sitti Abbas Mtemvu kujisalimisha kwa kujivua taji mwenyewe, mapya yameibuka na Ijumaa Wikienda lina mzigo mkononi!
Mapya
hayo yameibukia ndani ya Kanisa la Revelation Church lililopo
Buza–Kipera jijini Dar kwa Nabii Yaspi Bendera ambaye amezungumzia ishu
ya Sitti kujivua taji mwenyewe.“Alikuja
kwangu nikamwombea, akapata taji. Hata alipopata alikuja kushukuru,
nilimwambia aendelee kudumu kwangu hadi atakapokwenda kwenye taji la
dunia (Miss World) lakini hakufanya hivyo,
akawa haji tena.“Hivi,
nitoe mfano mmoja. Kama mtu akienda kwa mganga kuomba apewe dawa ili
apate ujauzito, akishapata akaenda kwa mganga mwingine kuomba amfanyie
dawa ili ujauzito huo usitoke. Je, siku ukitoka nani analaumiwa, mganga
wa kwanza au wa pili?”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni